Wezamtima@...

Dar es salaam, Dodoma, Tanzania

Sunday, March 8, 2020

UPANA WA ELIMU.


                       UPANA WA ELIMU.

           Kila swali katika dunia hii, 
         linaweza kujibiwa kwa majibu-   
          matatu yenye maana tofauti-
                            kabisa.


         Dunia inashangaza sana ,mpenzi mfuatiliaji wa blog hii, -hasa ukiangalia maajabu ambayo Muumba katuumba nayo katika akili zetu sisi wanadamu.

     Huwa tunazaliwa tukiwa na akili changa na kuanza kufundinshwa na kujifunza hadi mwisho wa maisha yetu ya duniani. Kumbe suala la kujifunza na kufundishwa ni suala endelevu hadi mwisho wa muda wa mwanadamu hapa duniani.

           Maarifa ni dimbwi la uchafu-
        ambapo mchanganyiko wa huo
     Uchafu,unaweza ukazalisha kitu -
           kizuri sana kiitwacho Elimu.


         Hauwezi ukawa na nidham ya hali ya juu sana ya kuogopa kutukana - kama hauyajui matusi yenyewe.

Hivyo basi maarifa huwa yamegawanyika, yaani mabaya na mazuri na kazi ya binadam ni kuchambua kipi anahitaji kukitenda maishani.

Ndugu yangu msomaji, mada yetu ni ndefu kidogo, hivyo najitahidi kuiweka kwa ufupi ili niguse kila kona ya ufahamu wako ipasavyo. 

Nadhani ushawahi kukutana na maswali yakakuchanganya ,hasa namna watu tofauti walivyokujibu na kila mmoja kwa maana na majibu tofauti kabisa. Na ukawa unajiuliza sasa ni yupi au n jibu lipi litakuwa sahihi.

Hapa ndo linakuja suala la upana wa Elimu kwa ujumla wake ,kwamba kuwa -kila swali lina majibu matatu yenye maana tofauti kabisa .majibu haya hujikita katika vipengele vitatu tofauti -navyo ni:-
  •  Maarifa ya jumla ya dunia
  • Maarifa ya uthibitisho wa imani
  • Maarifa ya upeo binafsi.
                 
Tuangalie mfano wa swali linavyojibiwa kwa hivyo vipengele vitatu juu.

   Mfano.  Kwanini maisha ni magumu?

                 Majibu.
       =maarifa ya jumla ya Dunia.
  
Maisha ni magumu kwa sababu watu walio wengi wanaishi bila utaratibu wa kujua kanunu  na siri za mafanikio .

   = maarifa ya uthibitisho wa imani. 

Maisha ni magumu kwa kuwa  baada ya binadamu kuasi katika busitani ya Edeni -alifunkuzwa na kutupwa duniani na Mungu akamuamulu kuwa ataishi kwa jasho lake. (-kwa uchungu utakula mazao yake siku zote za maisha yako. Mwanzo 3:17-18).

      =maarifa ya upeo binafsi.

Maisha ni magumu kwa sababu wanadamu hatuna nia ya dhati ya kusaidiana .


Nadhani umeona maarifa yalivyo gawanyika na umeanza kupata mwanga wa kusudi la mada yetu ya upana wa Elimu. Lakini nikwambie tu rafiki yangu kipenzi kwamba: maswali mengi watu hupenda kuyajibu kwa maarifa ya jumla ya dunia ,na mengine kwa maarifa ya uthibitisho wa imani, na ni Mara chache sana mtu kukujibu kwa maarifa ya upeo binafsi, na hapo ndo kwenye siri ya mafanikio ya mtu.





     ELIMU NI NINI?.

Elimu ni mfumo wa mafunzo yanayopatikana shuleni,vyuoni na maisha ni.

  Aina za Elimu - mfumo wa Dunia.

  • Elimu ya msingi
  • Elimu ya sekondari
  • Elimu ya  vyuoni.

  
  MAARIFA NI NINI?

Maarifa ni njia inayotumika kujitoa katika shida ama kuweza kupata kitu. Maarifa ni Elimu au ujuzi.

 Aina za maarifa katika Dunia.

  • Maarifa mazuri
  • Maarifa mabaya.


      -wazazi wanapaswa kuwafundisha-
   watoto wao namna ya kutafuta maarifa.
      Na sio tu inatosha kusisitiza watoto-
           wasimwache elimu aende zake.


 Kazi ya Elimu katika maisha ya  binadamu.

  • Kumlinda mwanadamu.
  • Kumwezesha apate anachokitaka.
  • Kutambua uwezo wa kipekee alionao.
  • Kumsaidia kutatua shida zinazomkabili.
  • Kurahisha maisha.

Kwanini wakati mwingine Elimu haiwasaidii walio nayo.

  • Ni namna tofauti walivyoipokea Elimu.
  • Nidhamu ndogo ya kuiishi Elimu waliyo nayo
  • Imani hafifu. Wengine wanaamini elimu walionayo ndo inafaa tu na ndo ya mwisho.
  • Mufumo wa elimu usiokidhi peo za kimataifa za kujitambua,kujitegemea na kujiajiri.
Upotoshaji kuhusiana na maana ya Elimu,kuwa ukisoma unakuwa na kazi nzuri na kupokea mshahara mkubwa.

         Chakufanya ili kuwa na Uhuru 
              wa Elimu na maarifa.

  1.  Kujitambua. Kujua maana ya Elimu, kuwa tunasoma ili kuongeza na kukuza peo zetu ili kurahisisha utatuaji wa changamoto zitakazotukabili.

  2.  Imani.kujiamini na kuamini uwezo wako wa ndani na kuendelea kuukuza kwa kujifunza na kutenda.

   3.mahusiano.Maarifa mazuri ni yale yanayonuai kuifanya dunia kuwa sehemu nzuri ya kuishi .

     4.  Ndoto/ malengo

  5.     Kujifunza.namna bora ya kufika kunako ndoto zako.

      6.  Anza sasa thubutu.


    
             Kinachomtofautisha mtu-
        mmoja na mwingine -sio akili au-
     bahati ya kuzaliwa.Bali ni mapokeo
             na matunizi ya Elimu na-
                Maarifa mbalimbali.

Nakushukuru kwa kufuatana nami hadi tamati ya mada yetu ,natumai umepata mwangaza mpya wa namna ya kuishi . karibu na endelea kufuatilia wezamtima@.. Kina cha fikra za utafiti na uzoefu wa maisha.


             Anthony Mwaka.
                  Mwandishi.
                Mujasiliamali.
                  Muuigizaji.

         Tel: +255738651846.
                 +255659594226.


              Wezamtima@gmail.com.


       Kina cha fikra hakina ukomo.





Thursday, November 21, 2019

NGUVU YA NAFASI YA MWISHO.



                    NGUVU YA NAFASI
                        YA MWISHO.


         Kama utafanya jambo kiasi-
           kwamba hautapata tena-
          nafasi nyingine kulifanya,
          hakika utakuwa mshindi ---
                 wa jambo hilo.

   
           Linapokuja swala la nguvu ya nafasi ya mwisho -kila mtu anaguswa kwa aina ya
kipekee kabisa -kwani kila mmojawetu kwa
nafasi yake alishawahi kupitia katika nafasi
ambayo ilikuwa ya mwisho kabisa kwenye
kuliteda jambo hilo.

Aidha kwa kujua au kutojua ,lakini hata wewe mwenyewe ulishapita kwenye nafasi fulani katika maisha yako na ukaona kama vile ni nafasi ya mwisho ya kutenda jambo hilo.

Mfano wa nafasi za mwisho tulizozipitia na tutakazozipitia katika maisha yetu ni kama vile:- siku ya mtihani wa mwisho kuhitimu elimu fulani,siku ya mashindano ya mchezo fulani, n.k.





Unaionaje nguvu/msukumo ambao huwa upo ndani yako ikiwa ni nafasi ya mwisho ya kutenda jambo hilo.na hautapata tena nafasi nyingine kulitenda jambo hilo maishani mwako .

             Hapa ndo utaona upekee wa binadamu, kila mtu huwa yupo tofauti akiwa na utulivu huku akiamini uwezo wake wa ndani na anachokijua.

Lakini siri uliokuwa haufahamu katika siku ya nafasi ya mwisho ni kwamba:-kuna nguvu ya aina ya kiutofauti ambayo huwa ndani ya mtu -humsaidia mtu kupambana
kadri awezavyo ili kushida.

Ndugu msomaji na mfuatiliaji wa wezamtima@.. -- nguvu hii ya nafasi ya mwisho inahitajika kutumika hata katika maisha ya kawaida ya kusaka mafanikio.

Amini nakuhakikishia kuwa kiu chako cha kufanikiwa kutimia --kinahitaji nguvu ya aina yake ya kujitoa kutafuata hayo mafanikio kiasi kwamba hautapata tena nafasi nyingine .

Kama utazamishwa ndani ya maji kwa dakika kadhaa hivi,na ukawa na kiu kubwa ya kutaka kuibuka na kuvuta hewa, kuhema,kiu hivyo ni sawa na nguvu ya nafasi ya mwisho.kama ulivyokuwa unaisaka nafasi ya kupata hewa/kuhema katika maji --kiu hivyo itumie na kutafuta mafanikio.

          SIFA ZA NGUVU YA NAFASI
                   YA MWISHO.

         1. USHINDI.
Mtu akipewa nafasi ya mwisho huhesabu kushinda ,huamini sana akili na uwezo wake.

      2.  UMAKINI.
Umakini huwa ni wa hali ya juu kuliko kawaida ya siku zote ,kuhakikisha kuwa hakuna kitu cha kukosea.

      3.  UWEZO.
Uwezo wa mtu wa ndani humfariji mtu na kumhakikishia kuwa anaweza kushinda.

       4.  UHAKIKA.
Imani isiyo ya kawaida huwa iko na mtu anapokuwa katika kuitumikia nafasi ya mwisho kufanya jambo.

      5.  UZINGATIVU.
Kama ni kanuni atazingatia ,yaani kila kitendo anachotenda atazingatia maelezo au kanuni maalumu.

     6.  UVUMILIVU.
Uvumilivu humjia kwa kiwango kisicho ukomo ,hawezi- choka kabla ya kuhitimisha jambo.

     7.  JITIHADA.
Liwalo na liwe lakini juhudi zote huziweka mtu katika siku ya nafasi ya mwisho.

    8.  UTII.
Hukubaliana na kila utaratibu na kuwa chini ya sheria ilimladi tu afanye kwa ufanisi jambo hilo.

   9.  UTEKELEZAJI.
Huwa hana mda mwingine tena wa kutekeleza jambo hilo ,hivyo fikra zote hufikiri na kutekeleza jambo hilo.


        Ndugu yangu napenda utambue kuwa maisha ya mafanikio sio kazi rahisi ,hivyo tunahitaji sana nguvu hii ya nafasi ya mwisho kutimiza malengo ya ndoto zetu.





        -Leo amua kushinda kila changamoto,
        Ili ufikie kilele cha ndoto yako.
                = Joeli Nanauka.


Ona kama ndo umepewa nafasi nyingine ya mwisho kutafuta mafanikio ya ndoto zako. Badili fikra ili kesho yako iwe nzuri .

           I am who I am to day because of -
          the decision i made yesterday.
              =Eleanor Rooselvelt.


    SABABU ZINAZOWAFELISHA WATU 
 WAKIWA KATIKA NAFASI YA MWISHO
           YA KUTEKELEZA JAMBO



  • Umakini mdogo wakuitumia nguvu ya nafasi ya mwisho
  • Wasiwasi unaotokana na upekee wa nafasi hii.
  • Kutokujiamini na kuogopa ushindani.
  • Kuwa na huzuni -iliyosababishwa na hali za kimaisha ,:- msiba ,nk.
  • Maandalizi madogo ukilinganisha na ukubwa wa nafasi hiyo ya mwisho.

Natumai tunaenda sambamba mwanaharakati wangu,uliye na fikra za kipekee kabisa juu maisha .najitahidi kufafanua bila kukuchosha ili ujue unahitaji hamasa,upeo na nguvu kiasi gani kufika unakotaka kwenda.

Sina la ziada nakuachia utajiri wa hiyo nguvu ya nafasi ya mwisho ,nadhani uhalisia wa maisha yako unaufahamu we we mwenyewe zaidi kuliko mimi. Hii ni nafasi nyingine ya mwisho uliopewa maishani mwako ,sidhani kama utaitumia vibaya. 



      Anthony  Elia Mwaka

               Mwandishi
              Mjasiriamali
                Muigizaji.


         Tel.no. +255659594226
                      +255738651846


        wezamtima@gmail.com


         www.wezamtima.com.

  Born-Dodoma, live-Dar es salaam.


     Kina cha fikra hakina ukomo.


Wednesday, November 13, 2019

KATA UTEPE - MBELE KWEUPE.


                         KATA UTEPE
                    MBELE KWEUPE

          Unavyoyatafsiri maisha -ndivyo
          utakavyo yaishi. Lakini  namna
            unavyofikiria kuhusu maisha,
                Ndivyo utakavyo-tenda.
                 Na matendo yako -ndio--
                 Yatakuwa maisha yako.


     
           Ebu nijaribu kukurudisha nyuma-------
miaka kumi ya maisha yako iliyopita ,kama
nigelikutana na wewe ningelikuuliza swali-hili:- "Hamisi --hivi miaka kumi ijayo utakuwa haumiliki hata ka-gari ka kutemb-elea?

Kwa uharaka na uhakika ungenijibu kuwa
miaka kumi ijayo ungekuwa unamiliki gari
Nzuri la kisasa, nyumba na mafanikio mengi tu ya ndoto zako.

Sasa mda huu mikaka kumi imeshakwisha
na nimekuja tayari tuone majibu uliyonijib-
u yametimia? Majibu unayo wewe mweny--
ewe kiukweli.

Kama majibu uliyonihakikishia kipindi kile
miaka kumi iliyopita yametimia unastahili
Pongezi lakini kama hakuna jipya lililojitok-
eza na maisha unayaona afadhali ya jana---,
Unahitajika kukata UTEPE, --habari njema
mbele ni KWEUPE.

Swali nalokuachia ktk siku ya Leo ni kwam-
ba:- unadhani miaka kumi ijayo jamii yako
na dunia kwa ujumla itajivunia nini kutoka
kwako?watu watakuhitaji kwa kiwango gan
i kutatua shida zao? .Kiukweli unahitajika
kukata utepe, ila habari njema mbele ni -----
kweupe.



          UTEPE NI NINI?
        Utepe ni ugwe(kamba)  wa kitambaa au
nguo. Tafsiri hii ni kwa mujibu wa kamusi
sanifu ya kiwahili. Kisanaa jinsi nilivyolitu--
mia neno utepe -ni ukanda kati yako na ------
kule unakoelekea(mafanikio).

Kukata utepe maana yake ni ni namna gani upambane na changamoto zinazokuzonga
ktk mambo hususani kama yafuatavyo:-


  • Ktk unachokifanya .
Inawezekana kuna changamoto kadha wa--
kadha ktk kazi yako ,ktk chochote unachokifanya siku hizi, ila tambua kuwa kila mtu aliyewahi kufanya unachofanya ---
alikumbana na changamoto mbali-mbali 
kama unazopitia wewe au nyingi hata wew
e haujazipitia.

Mara nyingi watu huona kama ni mikosi 
kupitia ktk changamoto ,ila tu nikwambie 
kuwa sio mikosi bali ndio utaratibu wa ----maisha ,changamoto zipo duniani na kila
 mtu atazipitia ,--lakini mchakato wa kutatua changamoto niendelevu hadi mwaisho wa uhai wetu duniani.

Leo kata utepe tafuta suluhisho la changa---
moto zinazokusumbua na sio kulalamika 
na kukata tamaa.

  • Ktk unachotamani kukifanya.
Kuna wakati huwa unaogopa kutoa maamuzi ya kufanya kitu cha ndoto zako
au biashara fulani au kitu kingine.kata utepe anza kufanya hakuna muda au wakat
i ambao utakuwa sahihi kufanya ,anza sasa.

  • Ktk kufilisika kwako.
Kufilisika ni kutokupata matokeo chanya kwa kileulichowekeza ,au kuplomoka kutoma juu ulipofikia hadi chini kiasi kwamba unaanze upya tena kwenda juu.

Kama hali hiyo imekukuta ,unachotakiwa kufanya ni kukubali kuwa umefilisika,pili,
kukata utepe na kuanza safari upya -kwani
una uzoefu wa hali ya juu.


  • Ktk woga.
Woga unawasumbua watu wengi sana maishani, ni kweli kuna vingi vya dunia vinatisha -kama vile:- magonjwa, njaa, umaskini, vita,nk. Lakini tu nikwambie ndugu msomaji kuwa, kuishi kwa kuogopa viogovya vyote vya dunia  --ni maisha mabaya zaidi kuliko unavyoviogopa.

Kata utepe ishi ukiwa huru kuanzia akilini
,moyoni na mwilini,kwani mbele kweupe.

  • Ktk maumivu.
Kwakuwa changamoto zitakujia maishani 
kwahiyo tambua kuwa kuna wakati utapita
Ktk maumivu, aidha usababishiwe au uyasababishe mwenyewe.

Kata utepe ,mbele ni kweupe ,maumivu uliyonayo ni ya muda mfupi tu .


  • Ktk uzingativu.
Kitu kinachokwamisha mafanikio ya watu
walio wengi ni:- kutokuwa na uzingativu 
ktk jambo moja ,bali wanajaribu kufanya kila kitu,kila fursa.

Kata utepe, wekeza nguvu na akili zako ktk kitu kimoja cha ndoto zako ,unachokitenda
Kutoka moyoni, utaona mbele ni kweupe.


   DHUMUNI KUU LA KUKATA UTEPE KTK 
                    MAKALA  HAYA.

        Dhumuni la makala haya ni kukutaka uelewe tafsiri halisi ya neno Maisha, na uchukue hatua za haraka kuweza kubadili fikra ili kufikia ndoto zako au kule
unakoelekea.

MAISHA NI NINI?
     Maisha ni muda wa uhai wa kiumbe. kwa mujibu wa tafsiri ya kamusi ya kiswahil sanifu.


Kumbe kila mtu ana maisha bila upendeleo
wowote ,tena maisha mazuri kabisa . kila binadamu kaubwa na Mungu kwa kusudi 
maalumu aje duniani aishi muda maalumu
, akamilishe jukumu maalumu.



Maisha hayahitaji uwe na wasiwasi kwa 
kila jambo ,ila yanahitaji utulize uwezo uliojaliwa,ulioumbwa nao na Mungu, uwezo huo ukusaidie ufike unapopataka kulingana na kusudi la Mungu na mpangilio wa ndoto zako.


  NAMNA YA KUKATA UTEPE NA KUONA 
         MBELE KULIVYO KWEUPE.


         1.  Kubadiri fikra.
Kila mabdailiko huanzia kichwani ktk fikra.
Kubali kuwa na fikra tofauti hasa kutoka kwa watu mbali-mbali ,kutana na watu ,soma historia za maisha yao, huzuria semina mbali-mbali za hamasa na mafanikio.nk.

      2.jua kusudi .
Tambua upo duniani kwa kusudi gani ,na una ndoto gani kutimilisha kusudi hill.

     3.tafsiri chanya .
Tafsiri chanya ndio mafanikio yenyewe ktk maisha ,matatizo yote hutatuliwa kwa mawazo chanya tu.

      4. Maono.
Ielekeze akili yako kwa tafsiri chanya kule kunako matamanio ya mafanikio yako.


     5.  Ndoto.
Usiishi ilimladi tu siku ziende ,ukishajua kusudi lako ,panga ndoto zako na uanze kuzitekeleza.

      6.  Mwelekeo.
Songa mbele kata utepe kueleke ndoto zako ziliko ,mbele kweupe ,changanua changamoto.

       7.  Jinsi ya kufika huko.
Umeshauona mwelekeo ,sasa utafikaje huko ,usijiulize sana ,anza safari tepe zitakuwa nyingi njiani ,kata moja moja ila habari njema ni kwamba--mbele ni kweupe.


Najivunia wewe unaefuatilia wezamtima@.., endelea kujionea majabu ya mabadiliko ya kimafanikio maishani mwako .


         By,Anthony Elia Mwaka.
   


          Mwandishi 
         Muigizaji
         Mujasiliamal.


        Tel. +255659594226
                +255738651846


       Wezamtima@gmail.com
   

Website=  www.wezamtima.com


Dodoma -Tanzania.



        Kina cha fikra haikina ukomo.


Sunday, November 10, 2019

UBORA NA UFANISI.



                       UBORA NA UFANISI.

           Mafanikio ni matokeo ya ubora na
             ufanisi kwa unachokitenda kwa
              kila siku bila kujali ugumu wa
               mazingira au maslahi binafsi.

            Nianze kwa kukuhusisha na simlizi ya kusisimua ya kijana mmoja aitwaye Lostam Magana.

            Lostam alikuwa akifanaya kazi ktk hali ngumu ya manyanyaso ktk mgahawa mmoja huko Temeke jijini Dar es laam.

Lostam alipata kazi hiyo baada ya kuteseka sana na hali ya utoto wa mtaani kwa zaidi ya mika kumi tangu mama yake afariki dunia na kumuacha na umri wa miaka nane huku akiachwa hana baba kwani mama yake alikuwa mwathilika wa
madawa ya kulevya (teja) --hivyo hakujua wala hakujali aliupata wapi ujauzito wa Lostam.

Lostam alilelewa mtaani pamoja na watoto wenzake wa mtaani ktk mazingira yasiyoelezeka (magumu) hadi alipokua na kupata kazi ktk mgahawa fulani huko Temeke jijini Dar es salaam.



Licha ya Lostam kuona kama ahueni ya maisha mgahawani kuliko ya mtaani -lakini
bado alikuwa kakumbwa na zongo la manyanyaso na ugumu wa maisha.

Alitumikishwa kazi kupita kiasi ,yaani alala saa sita usiku na kuamka saa tisa kwaajiri ya kazi kwa ujira wa 2500Tsh kwa siku.

Lostam hakukata tamaa aliendelea kujitu-
ma na kuonesha ubora na ufanisi wake ktk kazi ,alitii na kufuata masharti yote ya msimamizi wa mgahawa huo licha ya kupitia ktk mazingira magumu.

         Siku moja mmiliki(boss) wa mgahawa huo alitembelea mgahawani kwake ,-ilikuwa ni miezi saba baada ya Lostam kuajiriwa pale mgahawani.

Siku hiyo Lostam aliamlishwa na msimamizi wa mgahawa huo kuwa amhudumie boss wao , Lostam alitii kama ilivyo kawaida yake na ubora wake na ufanisi akamhudumia boss.

Baadae akaitwa na boss na kuambiwa kuwa tangu siku hiyo ndio mwisho wa kufanya kazi ktk mgahawa ule.kwani boss alivutiwa na ufanisi wake ktk kazi na akaamua kumpeleka moja ya hoteli zake kubwa  kulingana na ubora na ufanisi wake.

Tangu siku ile Lostam akaandika ukurasa mpya wa maisha yake - hadi navyoandika makala haya sasahivi -Lostam ni meneja  msaidizi wa hoteli zote zinazomilikiwa na huyo boss.




          UBORA NA UFANISI NI NINI?

      Labda unajiuliza maana na tafsiri ya maneno haya mawili yanayotikisa kurasa za makala haya.

UBORA ni thamani ya kitu au hali ya upekee isiyofananishwa na ya kitu kingine.

UFANISI ni ya kupatikana kwa mafanikio au usitawi.

Kwahiyo maana ya ubora na ufanisi ni thamani ya usitawi wa mafanikio fulani .



        Thamani hii ya usitawi wa mafanikio fulani hujengwa na matendo ya mtu ya kila siku. Je huwa unafanya mambo kwa kuangalia maslahi tu? au kwa kuangalia Leo tu?.

Unapofanya vizuri kwa viwango vya juu bila kujali ugumu wa mazingira au maslahi unajiwekeea utayari wa mafanikio mbeleni ,amini nakwambia unachokitoa ni lazima uje kukipokea -hata kama kitachelewa .

 Nimnukuu mhamasishaji wa kujitambua na mwandishi nguli wa vitabu nnchini Tanzania ,-alisema:-

    1.    "Wengi wetu tunataka utukufu,laki--
ni hatutaki safari ya kuelekea utukufu huo".
             =Eric Shigongo.

   2.   " bahati hujengwa na binadamu mwenyewe ,unapofanya kazi kwa nguvu zaidi ndivyo unavyopata bahati zaidi ya kufanikiwa".
               =Eric Shigongo.

Chochote unachofanya Fanya kwa ubora na ufanisi wako wote utakuwa unajiweka kwenye bahati ya kufanikiwa, mafanikio yoyote yale ni matokeo ya nguvu ya ubora na ufanisi wa matendo yaliyopita.

     MAMBO YA KUFANYA ILI UWE BORA                               NA MFANISI

   1.  Fikiri kabla ya kutenda.
Kumbuka matendo unayoyatenda ndio maisha yako ya kesho, tathimini na uangalie faida ya kesho ya matendo hayo.

   2.   Jione unaweza hata pasipo na njia.
Uwezo wako haushindwi kitu ,fikra hazina ukomo ,chochote unachotaka kimo.

   3.    Waza chanya.
Usiruhusu wala kuangalia yale mambo hasi ,bali zingatia mambo chanya bora ya kukujenga ,kwani matatizo yote hutatuliwa kwa fikra chanya.

   4.       Kuwa wa viwango.
Yaani sio mtu wa kawaida wala haufananishwi na yeyote duniani ,na kila unachokifanya unafanya kwa ustadi wa hali ya juu sana,haijalishi kitu hicho kidogo au kikubwa.

    5.      Uwe wa pekee.
Wewe ni wewe tu ,utambulisho wako ni namna ulivyo bora na mfanisi ktk matendo yako yote .

     6.       Jitoe .
Kujitoa ni hali ya kung'ang'ania jambo na kuamini litatokea ,na kufanya hadi upate matokeo uliyoyakusudia.

     7.     Jitathimini.
Wote walio bora na wafanisi hujitathimini na kujipongeza kwa mazuri waliyofanya ,kuupa mwili na akili ushindi wa kufanya na mambo mengine kwa ubora na ufanisi.
Kujitathimini pia hugundua makosa na kasoro zako na kujilekebisha.

      8.     Jifunze.
Kujifunza ni jambo endelevu ,usipojifunza kila kukicha - utaachwa mbali sana na dunia hii inayoenda kasi na ushindani wa maarifa.

        9.  Amini na uifuatilie imani yako.
Isiwe  tu kuwa we we ni mtu wa imani fulani --lakini ukawa hauijui imani yako - ni hasara. Mtoto yatima hujiona ni mpweke na asiye na usalama kuliko yule mwenye wazazi. Ukijifungamanisha ktk imani yako utajiona usiyeteteleka .

         10.   Tekeleza.
Hata uendele kujifunza vipi ,kama hauchukui hatua za uthubutu na utekelezaji hauwezi pokea mabadiliko ktk maisha yako.

        Sina la ziada ,nashukuru kuwa nawe na endelea kunifuatilia mpaka maisha yaimalike ktk mafanikio.


           By, Anthony Elia Mwaka.

                       Mwandishi
                       Mjasiriamali
                       Muigizaji.

             Tel. +255659594226
                     +255738651846

 
                 Wezamtima@gmail.com

             Websites, www.wezamtima.com

                   Dar es salaam--Tanzania


                Kina cha fikra hakina ukomo.






Tuesday, November 5, 2019

RAFIKI WA MAFANIKIO NI TABIA.


          RAFIKI WA MAFANIKIO NI TABIA.

          Haijalishi ni matokeo chanya au
          hasi --yote hutokana na tabia za
          kila siku zinazotendwa na mtu .

         
                Uumbaji wake Mungu kwa mwan--
adamu ulibuniwa kwa mfumo wa ufanisi ---
wa kipekee sana. Yaani namna mfumo mn--
zima wa mwili unavyofanya kazi kwa mpa-
ngilio unaojiendesha wenyewe.

Wataalam na watafiti wa masuala ya mifumo ya mwili wa mwanadamu wanasema kuwa - tabia ya mtu inayoanzia
ndani hutoka nje na kumpa vitendo,vitendo
hivyo hunukuliwa na mwili,ubongo na sehem za hisia ,hutengeneza muunganiko wa ushirikiono ktk kile kitendo . Nacho huwa ni tabia ya kila siku.

              TABIA.
          Tabia ni nini?
 Tabia ni mazoea yanayotokana na kurudia
rudia hali,mwenendo au matendo.

              MAFANIKIO.
       Mafanikio ni nini!?
 Mafanikio ni matokeo mazuri ya jambo
lililokusudiwa au halikukusudiwa.

       Kwahiyo tunaposema rafiki wa mafanikio ni tabia maana yake ni :- tabia
zako za kila siku ndizo zitaleta matokeo ,
ambayo ndio mafanikio yako.

Ila inabidi ufahamu kuwa ,kama una tabia
ambazo si rafiki wa mafanikio yako ,ujue
kuwa hutafanikisha unachokitaka.



            Kanuni iko hivi:-

  •    Mtu(m)
  •   Tabia(t)
  • Matokeo(mt)
  • Mafanikio (mf).

                  M+t=mt
                  Mt+t=mf(chanya au hasi)

Kwa hiyo kama umenielewa vema mpenzi
msomaji --usiendelee kulalamika au kulaumu watu juu ya mafanikio yako, bali
amua kujenga tabia ambazo zitakuwa rafiki
na mafanikio yako ,na uzitende kilazoea kw
a kila siku.


    NJIA ZA KUJENGA TABIA RAFIKI NA 
                 MAFANIKIO YAKO.


          1.  Kuwa na fikra chanya.
Yachukulie maisha yako ni wajibu wako na
wew ndo mwenye kuwajibika kwa kiwang-
o chote. Fikra chanya hujenga picha nzuri 
na matokeo mazuri --kwani -utakachokifik-
iri na kukitenda ndicho mafanikio yako.

        2. Malengo na malengo.
Bila mpango au lengo -hakuna unachokifanya.
             Jiwekee malengo yako ya ndoto zako
Kuelekea kule unakotaka kufika.

          3.   Kiu ya utekelezaji.
Jitoe kwa dhati kutekeleza unayojipangia,
maisha unayotaka uishi .

         4.  Bajeti.
Watu wengi wanaishi kama kuku ilimladi 
liende ,hawatako kujichosha,akipata hela 
anatumia tu bila na utaratibu maalumu.
Hakikisha unajua kila sh yako inatumikaje 
maana usije ukatuletea hadithi za usemi--
huu:- (napata tu hela ila sijui zinakoenda).

        5. Takwimu.
Kuwa na kumbukumbu ya mambo yako yote juu ya maisha yako.

         6.  Mtandao wa watu.
Hakuna mafanikio bila watu, jifunze namna ya kuishi na watu vema ili upate
wa kukushika mkono huko uendako.

          7. Uwekezaji.
Ni njia ya kipekee sana wanayoitumia watu wengi wanaofanikiwa .

          8.  Uthubutu.
Hakuna muoga aliyefanikiwa ,huu ni ulim--
wengu wa majasiri tu, umakini ni kitu cha 
msingi zaidi, Fanya kitu tuone.

         9. Ratiba.
Yaandike mambo mhimu ya kufanya kesho 
leo kabla ya kulala --na kesho uyatimize kama ulivyopanga katka ratiba yako.
Tafakar siku yako na ujipongeze na kujilekebisha unapoona umeenda sivyo.

      10.Utekelezaji.
Tekeleza yote unayoyapanga maishani mw-
ako kwa maana ndio ushindi wako wa mafanikio.



        Ndugu msomaji -maisha ni kupanga
na kuchagua kipi kiwe kipaumbele.naamin
kila mtu huwa ana hitaji la mafanikio ili 
aishi kwa fulaha, lakini itakuwa bora zaidi
kama utaanza na kuitafuta furaha halafu --
iende sambamba na mafanikio.



        MISINGI YA MAISHA YA FURAHA.
  • Upendo
  • Uadilifu
  • Ushirikiano
  • Unyenyekevu
  • Uwajibikaji
  • Ukarim  n.k.

Natumai tumeenda sambamba vizuri mno
na hongera kwa kunifuatilia,endelea kuwa 
karibu na wezamtima@... uzidi kuimalika.


           Anthony Elia Mwak


                  Mwandishi
                  Muigizaji
                  Mjasiriamali


           Wezamtima@gmail.com

           www.wezamtima.com

          Tel.  +255659594226
                   +255738651846


         Dar es salaam =Tanzania.


        Kina cha fikra hakina ukomo.





Wednesday, October 30, 2019

FIKRA ZA DHAHANIA


                 FIKRA ZA DHAHANIA

             Mwonekano wa maisha ya mtu
             ya sasa -upo kama alilivyokuwa
               akiwaza na kutenda mawazo-
                     hayo wakati uliopita.



             Ubongo wa mwanadamu umebeba
maajabu mazito mno,ubongo ndiyo kiongo-
zi mkuu wa maisha ya mtu. Ubongo hushirikaiana na milango ya fahamu, moyo
,na viamshi vingine vya hisia kumpa mtu----
mwonekano halisi wa maisha.

Milango ya fahamu pua,masikio,macho,nk.-
hukusanya taarifa fupi na kuzipeleka katik
ubongo kupitia neva ili taarifa hizo zikataf--
Siriwe -na zikishatafsiriwa hurudishwa ktk
mwili ,pia ubongo huamulisha mwili ufanye kitendo kulingana na jinsi ulivyotaf-
siri taarifa.

Kwahiyo ukiangalia kwa kina utagundua---
kuwa kumbe mwili hufanya kazi kama hali-
mashauli,(yaani kwa ushirikiano wa ajabu),
ukiongozwa na ubongo.

Nachotaka ujue hapa ni kwamba, uwe mak-
ini sana ktk kuutumia ubongo kutafsiri taar
-ifa, maisha yako yatazid kuimalika zaidi ---
kama utafsiri taarifa nyingi ktk hali chanya
kuliko hasi.

Eneo hili ndio kiini cha maisha na ndipo --
tunapotofautiana kati ya binadamu mmoja
na mwingine.

Ktk dunia hii utakutana na taarifa za kila --
aina,nzuri na mbaya -lakini kama hautawe-
za kupembua ktk hali chanya ujue kuwa ni
lazima tu utakuwa mtumwa wa fikra zako.

              Akili ina upana sana ktk kufikiria, ---lakini ktk fikra kuna fikra za dhahania na--
fikra za kawaida. Nadhani ulishawahi kuw-
aza vitu mpaka wewe mwenyewe ukawa   --
hauna uhakika kama yatatimia uyawazayo.


  • FIKRA ZA DHAHANIA . 
Fikra za dhahania ni nini?

               Fikra za dhahania ni mawazo ya --
kina yanayopambanua vitu visivyo oneka--
na, shikika wala kudhibitika.

Watu wengi wanateswa na fikra hizi wana-
waza maisha kwa kina kisichofikika na ku-
ona kama ni muuzija tu wengine kufaniki-
wa na wengine kuwa maskini kimaisha.

Kama unawaza vitu ambavyo hautaweza 
kuwaelezea watu wengine hazarani bila ya
aibu ama uwoga - basi vitu hivyo havitatokea.

Maisha sio bahati,miujiza,wala nyota. Bali--
ni namna unavyongoza mwili na akili yako ambavyo tayari Mungu alikwisha viumba,
na wewe ndio deleva.

Mafanikio yoyote yanatoka ktk fikra sahihi zilizotokana na taarifa unazopokea,tafakari
na tengeneza mfumo wa maisha wa kawaida tu wala usiwaze sana ,ila kuwaza ni jambo jema sana.waza ktk hali chanya --
na tenda zaidi.

   HASARA ZA FIKRA ZA DHAHANIA     

  • Utumwa wa fikra.
  • Sononeko la moyo(mfadhaiko).
  • Kukata tamaa.
  • Ulemavu wa fikra.
  • Kupoteza imani.
  • Kulaumu watu.
  • Upweke.
  • Kutokutimiza ndoto.
           HATUA ZA KUEPUKA FIKRA 
                     ZA DHAHANIA

           1. Kiasi.
Kuwa na kiasi kwa kila jambo unalofikiria 
na kutenda.kutokuwa na kiasi hupelekea 
ulevi na utumwa wa fikra.

            2. Mfumo.
Weka mfumo wa maisha ukuongoze ,yaani
amua unaishi maisha ya aina gani na uyaishi kwa furaha bila kuvunja heria.

           3.Vipaumbele.
Pangilia mambo yako na uyaweke ktk kuyatenda kulingana na umuhimu wake.

            4.Ratiba.
Moja ya njia zinazowafanikisha watu ni--
kuwa na ratiba ya siku na kuifuata hiyo --
Ikuongoze kwa siku nzima.

           5.kujitathimini.
Ukishakuwa na ratiba  ya siku yako-
mwisho wa siku yako - kaa chini uitafakari siku yako ulivyoipeleka kulingana na ratiba
yako. Jitathimini na ujipongeze na ujirekebishe ulipokosea .

        Sina la ziada mpezi mfuatiliaji wa makala haya ya WEZAMTIMA. Hongera sana kuwa nami na endelea kubadiri fikra
Ndani ya mgodi huu.


        Anthony Elia Mwaka

               Mwandishi-
               Muigizaji
               Mjasiriamali


        Tel.  +255659594226
                 +255738651846
  

          Wezamtima@gmail.com

      Website- www.wezamtima.com.


          Dar es salaam - Tanzania.


        Kina cha fikra hakina  ukomo.


Monday, October 28, 2019

RASILIMALI WATU

                 
                RASILIMALI WATU.

           Binadamu wote tunategemeana-
             kamwe hauwezi kufanikiwa-
                   bila kuwa na watu.


           Siku moja nilikuwa nasikiliza moja ya hotuba za baba wa taifa - mwalim- Julias Nyerere , nikamsikia akisema "ukimchukuwa mtu mmoja mwenye akili Sana na umpeleke katika kisiwa akaishi peke yake - mtu huyo hata pata maemdeleo yoyote".

Akaendelea kusema kuwa -maendeleo huletwa na watu na sio na mtu mmoja, ijapokuwa mtu mmoja anaweza kurudisha nyuma maendeleo yaliyotafutwa na watu wengi.

           Nisikutoe nje sana ya mada yetu (rasilimali watu) ,kwanza tujue maana ya rasilimali watu.

Rasilimali watu ni watu wote walioko chini ya umiliki,na usimamizi wako kwa unachokifanya.

Watu hawa wamegawanyika ktk makundi mawili nayo ni kama yafuatavyo:-

         1.  Watu wanaozalisha na kutoa-
               huduma.
        2.    Watu wanaopokea bidhaa au
               huduma.

Rasilimali watu ni moja ya rasilimali kuu ya
muhimu sana kwa wanahalakati wa mafa---
nikio,kwa maana binadamu tunategemea---
na katika kuyaendesha maisha.

Mafanikio yako yako mikononi mwa watu
ni namna gani unatengeneza miundombin
u za kuwashawishi watu wakuletee hicho-
unachokihitaji.

Amini ndugu - kila mtu unayemuona na usiye muona wote wameyabeba mafanikio yako wanasubiri utayari wako wakuletee
Mafanikio yako.

     MBINU ZA KIPEKEE ZA KUTENGENEZA
           RASILIMALI WATU YA KUDUMU.

           1:  aina ya wewe ulivyo.
Uwe wa aina fulani unavyotaka uwe kwa
watu na uishi hivyo,huku ukiwa sawa ----
Katika mizani -unapopimwa na watu ktk
dhana zifuatazo:-
                     *uaminifu
                     *busara
                     *hekima
                     *maono
                     *upendo.

          2:  kutatua changamoto za watu.
Dhumuni lako lisiwe ni kutafuta fedha ktk
dunia hii --fedha ni matokeo tu ya kutatua
kwa ufanisi changamoto za watu.

Matajiri wakubwa duniani ni wale wanao-
tatua shida za watu wengi sana ,kumbuka kiwango cha mafanikio kinategemea jinsi
watu wanavyokuitaji katika maisha yao.

            3:   Wajali watu.
Ishi na watu namna walivyo -bila kuwabagua kwa elimu zao,umaskin,utajiri
,rangi,au imani zao.kauli mbiu yako kila---
siku iwe ni jinsi gani unavyowaonea huduma watu wanavyoteseka na unafikilia
namna ya kuwasaidia.

           4:  Ubora wa ufanisi wa mifumo.
Tengeneza miundombinu rafiki kwa watu
bila kuwanyonya ,lakini wasaidie watu kwa
kupitia jasho lao,unachotoa -uwe umekwi--sha fikiria kitakavyorudi.

           5:  Maarifa.
Dunia inaenda kasi na mabadiliko ya kila
aina ya mitindo na mwingiliana wa --------
maarifa.jifunze ujuzi mpya na pia wafundishe wanaokufanyia kazi. wahudumiwa wako watataka utofauti na
mabadiliko.


        Sina la ziada ndugu msomaji -hongera
Sana kunifuatilia ,ila kizur kula na nduguyo
watu wanahangaika kwa kukosa maarifa na wanaona mafanikio ni kama miujiza tu.
Ebu waokoe kwa kuwaonesha blog hii.


         Anthony Elia Mwaka

kazi-mjasiliamali,mwandishi,muigizaji.

        Tel- no:- +255659594226
                       +255738651846

         Wezamtima@gmail.com

           www.wezamtima.com

     Kina cha fikra hakina ukomo.




UPANA WA ELIMU.

                        UPANA WA ELIMU.            Kila swali katika dunia hii,           linaweza kujibiwa kwa majibu-            ...