Wezamtima@...

Dar es salaam, Dodoma, Tanzania

Wednesday, October 30, 2019

FIKRA ZA DHAHANIA


                 FIKRA ZA DHAHANIA

             Mwonekano wa maisha ya mtu
             ya sasa -upo kama alilivyokuwa
               akiwaza na kutenda mawazo-
                     hayo wakati uliopita.



             Ubongo wa mwanadamu umebeba
maajabu mazito mno,ubongo ndiyo kiongo-
zi mkuu wa maisha ya mtu. Ubongo hushirikaiana na milango ya fahamu, moyo
,na viamshi vingine vya hisia kumpa mtu----
mwonekano halisi wa maisha.

Milango ya fahamu pua,masikio,macho,nk.-
hukusanya taarifa fupi na kuzipeleka katik
ubongo kupitia neva ili taarifa hizo zikataf--
Siriwe -na zikishatafsiriwa hurudishwa ktk
mwili ,pia ubongo huamulisha mwili ufanye kitendo kulingana na jinsi ulivyotaf-
siri taarifa.

Kwahiyo ukiangalia kwa kina utagundua---
kuwa kumbe mwili hufanya kazi kama hali-
mashauli,(yaani kwa ushirikiano wa ajabu),
ukiongozwa na ubongo.

Nachotaka ujue hapa ni kwamba, uwe mak-
ini sana ktk kuutumia ubongo kutafsiri taar
-ifa, maisha yako yatazid kuimalika zaidi ---
kama utafsiri taarifa nyingi ktk hali chanya
kuliko hasi.

Eneo hili ndio kiini cha maisha na ndipo --
tunapotofautiana kati ya binadamu mmoja
na mwingine.

Ktk dunia hii utakutana na taarifa za kila --
aina,nzuri na mbaya -lakini kama hautawe-
za kupembua ktk hali chanya ujue kuwa ni
lazima tu utakuwa mtumwa wa fikra zako.

              Akili ina upana sana ktk kufikiria, ---lakini ktk fikra kuna fikra za dhahania na--
fikra za kawaida. Nadhani ulishawahi kuw-
aza vitu mpaka wewe mwenyewe ukawa   --
hauna uhakika kama yatatimia uyawazayo.


  • FIKRA ZA DHAHANIA . 
Fikra za dhahania ni nini?

               Fikra za dhahania ni mawazo ya --
kina yanayopambanua vitu visivyo oneka--
na, shikika wala kudhibitika.

Watu wengi wanateswa na fikra hizi wana-
waza maisha kwa kina kisichofikika na ku-
ona kama ni muuzija tu wengine kufaniki-
wa na wengine kuwa maskini kimaisha.

Kama unawaza vitu ambavyo hautaweza 
kuwaelezea watu wengine hazarani bila ya
aibu ama uwoga - basi vitu hivyo havitatokea.

Maisha sio bahati,miujiza,wala nyota. Bali--
ni namna unavyongoza mwili na akili yako ambavyo tayari Mungu alikwisha viumba,
na wewe ndio deleva.

Mafanikio yoyote yanatoka ktk fikra sahihi zilizotokana na taarifa unazopokea,tafakari
na tengeneza mfumo wa maisha wa kawaida tu wala usiwaze sana ,ila kuwaza ni jambo jema sana.waza ktk hali chanya --
na tenda zaidi.

   HASARA ZA FIKRA ZA DHAHANIA     

  • Utumwa wa fikra.
  • Sononeko la moyo(mfadhaiko).
  • Kukata tamaa.
  • Ulemavu wa fikra.
  • Kupoteza imani.
  • Kulaumu watu.
  • Upweke.
  • Kutokutimiza ndoto.
           HATUA ZA KUEPUKA FIKRA 
                     ZA DHAHANIA

           1. Kiasi.
Kuwa na kiasi kwa kila jambo unalofikiria 
na kutenda.kutokuwa na kiasi hupelekea 
ulevi na utumwa wa fikra.

            2. Mfumo.
Weka mfumo wa maisha ukuongoze ,yaani
amua unaishi maisha ya aina gani na uyaishi kwa furaha bila kuvunja heria.

           3.Vipaumbele.
Pangilia mambo yako na uyaweke ktk kuyatenda kulingana na umuhimu wake.

            4.Ratiba.
Moja ya njia zinazowafanikisha watu ni--
kuwa na ratiba ya siku na kuifuata hiyo --
Ikuongoze kwa siku nzima.

           5.kujitathimini.
Ukishakuwa na ratiba  ya siku yako-
mwisho wa siku yako - kaa chini uitafakari siku yako ulivyoipeleka kulingana na ratiba
yako. Jitathimini na ujipongeze na ujirekebishe ulipokosea .

        Sina la ziada mpezi mfuatiliaji wa makala haya ya WEZAMTIMA. Hongera sana kuwa nami na endelea kubadiri fikra
Ndani ya mgodi huu.


        Anthony Elia Mwaka

               Mwandishi-
               Muigizaji
               Mjasiriamali


        Tel.  +255659594226
                 +255738651846
  

          Wezamtima@gmail.com

      Website- www.wezamtima.com.


          Dar es salaam - Tanzania.


        Kina cha fikra hakina  ukomo.


Monday, October 28, 2019

RASILIMALI WATU

                 
                RASILIMALI WATU.

           Binadamu wote tunategemeana-
             kamwe hauwezi kufanikiwa-
                   bila kuwa na watu.


           Siku moja nilikuwa nasikiliza moja ya hotuba za baba wa taifa - mwalim- Julias Nyerere , nikamsikia akisema "ukimchukuwa mtu mmoja mwenye akili Sana na umpeleke katika kisiwa akaishi peke yake - mtu huyo hata pata maemdeleo yoyote".

Akaendelea kusema kuwa -maendeleo huletwa na watu na sio na mtu mmoja, ijapokuwa mtu mmoja anaweza kurudisha nyuma maendeleo yaliyotafutwa na watu wengi.

           Nisikutoe nje sana ya mada yetu (rasilimali watu) ,kwanza tujue maana ya rasilimali watu.

Rasilimali watu ni watu wote walioko chini ya umiliki,na usimamizi wako kwa unachokifanya.

Watu hawa wamegawanyika ktk makundi mawili nayo ni kama yafuatavyo:-

         1.  Watu wanaozalisha na kutoa-
               huduma.
        2.    Watu wanaopokea bidhaa au
               huduma.

Rasilimali watu ni moja ya rasilimali kuu ya
muhimu sana kwa wanahalakati wa mafa---
nikio,kwa maana binadamu tunategemea---
na katika kuyaendesha maisha.

Mafanikio yako yako mikononi mwa watu
ni namna gani unatengeneza miundombin
u za kuwashawishi watu wakuletee hicho-
unachokihitaji.

Amini ndugu - kila mtu unayemuona na usiye muona wote wameyabeba mafanikio yako wanasubiri utayari wako wakuletee
Mafanikio yako.

     MBINU ZA KIPEKEE ZA KUTENGENEZA
           RASILIMALI WATU YA KUDUMU.

           1:  aina ya wewe ulivyo.
Uwe wa aina fulani unavyotaka uwe kwa
watu na uishi hivyo,huku ukiwa sawa ----
Katika mizani -unapopimwa na watu ktk
dhana zifuatazo:-
                     *uaminifu
                     *busara
                     *hekima
                     *maono
                     *upendo.

          2:  kutatua changamoto za watu.
Dhumuni lako lisiwe ni kutafuta fedha ktk
dunia hii --fedha ni matokeo tu ya kutatua
kwa ufanisi changamoto za watu.

Matajiri wakubwa duniani ni wale wanao-
tatua shida za watu wengi sana ,kumbuka kiwango cha mafanikio kinategemea jinsi
watu wanavyokuitaji katika maisha yao.

            3:   Wajali watu.
Ishi na watu namna walivyo -bila kuwabagua kwa elimu zao,umaskin,utajiri
,rangi,au imani zao.kauli mbiu yako kila---
siku iwe ni jinsi gani unavyowaonea huduma watu wanavyoteseka na unafikilia
namna ya kuwasaidia.

           4:  Ubora wa ufanisi wa mifumo.
Tengeneza miundombinu rafiki kwa watu
bila kuwanyonya ,lakini wasaidie watu kwa
kupitia jasho lao,unachotoa -uwe umekwi--sha fikiria kitakavyorudi.

           5:  Maarifa.
Dunia inaenda kasi na mabadiliko ya kila
aina ya mitindo na mwingiliana wa --------
maarifa.jifunze ujuzi mpya na pia wafundishe wanaokufanyia kazi. wahudumiwa wako watataka utofauti na
mabadiliko.


        Sina la ziada ndugu msomaji -hongera
Sana kunifuatilia ,ila kizur kula na nduguyo
watu wanahangaika kwa kukosa maarifa na wanaona mafanikio ni kama miujiza tu.
Ebu waokoe kwa kuwaonesha blog hii.


         Anthony Elia Mwaka

kazi-mjasiliamali,mwandishi,muigizaji.

        Tel- no:- +255659594226
                       +255738651846

         Wezamtima@gmail.com

           www.wezamtima.com

     Kina cha fikra hakina ukomo.




Saturday, October 19, 2019

UFAHARI WA KUJITAMBUA.

               UFAHARI WA KUJITAMBUA.

     Umasikini wa kiwango cha juu kabisa-
     ni ule wa kutokuijua thamani   --yako-
                      Na upekee wako.


          Ufahari wa kujitambua ni nini?,najua-
unazijua fahari nyingi sana za hapa dunian
i ,kama :- majumba, magari, ndege, na mafanikio mengine makubwa tu -nayo Yote
ni fahari za hapa duniani.

          Lakini leo ni siku ya kipekee mno ili--
tujifunze huu ufahari wa kujitabua ni ufahaari wa aina gani.

Ufahari wa kujitambua ni sentensi iliyojengwa kwa maneno makuu mawili nayo ni  --ufahari (fahari)
                --kujitambua (tambua).

  • Neno (fahari) maana yake ni "ukuu/utukufu---jambo au kitu cha sifa cha kujivunia kwa watu". 

Na neno (tambua) maana yake ni "kukumbuka au kujua  uasilia wa kitu au jambo fulani". Hii ni kwa mujibu wa tafsiri ya kamusi ya kiswahili sanifu.

            Kwahiyo kwa ujumla maana ya sentensi ufahari wa kujitambua ni kujua----
Utukufu /ukuu /thamani/upekee --ambao kiasilia uliumbwa nao na haufanani na wa
mtu yeyote yule.

Kujitambua Sio jambo la kawaida kama unavyodhani,  jua kuwa -kinachotutofautisha wanadamu -mmoja na mwingine ni namna tunavyojitambua.

Wale wanaojitambua zaidi ndio wanaofanikiwa zaidi maishani, na wasio jitambua -utashangaa Mpaka wanakuwa wazee kabisa lakini hawajafanikiwa na hawana hata fahari yoyote ya kujivunia.

   Njia yakinifu za kujitambua mwenyewe
   na kuanza kunufaika na fahari hii ya ku-
   jitambua, kama fahari yako ya kwanza---
                  ya Muhimu duniani.

1. Asili yako.
 Ijue asili yako, umezaliwa wapi, mna utamaduni na desturi gani, ni nini vya thamani mnavyojivunia kwenu. Kumbuka wanaofanikiwa duniani ni wale wanaofanikiwa kuutangaza utamaduni. Wao na kuuuza.

2. Upeo na vipaji vyako.
Usijidharau na kujiona huwezi kwa namna ulivyo, Mungu kakuumba na uwezo wa kipekee ambao haufanani na wa mtu yeyo-
te yule duniani. Tambua vipaji vyako na Fanya unavyoona inafaa bila kuangalia watu watasemaje --ilimladi tu usivunje maadili na sheria za nchi.

3. Kujifunza.
Kujifunza ni jambo la msingi na endelevu
Katika kukuza na kuendeleza kujitambua kwa mtu. -- ukijifunza kwa kila mtu unaeonana nae, kutananae --basi wewe hautakosea,.
                  --- Jifunze kwa kusoma vitabu --kama unavyofanya muda  huu, Kuna nguvu ya pekee sana katika kujisomea.
                 ---- Jifunze kwa kusikiliza na kutazama pia vitendo mbalimbali vya watu.

4. Ishi upeo wako.
Kuiiga ni jambo zuri tu -kama unaiga chenye manufaa, usiishi maisha ya kuigiza tu kila kitu, kuwa na maisha asilia ya kwako peke yako kwa maana ndicho kitakachokuwa utambulishao wako. Na ita-
kuwa fahari kwako Kama watu wataiga upekee wako.

5. Tekeleza majukumu yako.
Usiishi kwa kushindana na watu, ama usitafute mafanikio ili umpite fulani, hapana.
Fanya unachofanya ili kutimiza majukumu ya maamuzi yako uliyoyatoa. kwa ujumla shindana na majukumu yako.


         Kamwe hautalalamika hata siku moja kuwa Wewe ni maskini kama tu utakuwa umejitambua, fahari ya kujitambua ndio fahari ya kwanza ambayo mtu anatakiwa awe anaifahamu. Ebu anza na kuitafuta fahari Hiyo fahari nyingine zitakuja zenyewe.


Wezamtima@..tumejidhatiti kwa dhati kabisa kuhakikisha watu wengi wanajitambua na kuendana na dunia ya sasa, inayoenda kasi ikiwa imejawa na ushindani wa maarifa.

Karibu sana utaendelea kunufaika na machapisho mengine ya tija ya kutukomboa maishani --kizuri kula na nduguyo -usiwe mchoyo washirikishe na wengine wapate maarifa Haya.


  Anthony Elia Mwaka


Mwandishi,mjasiliamali,muigizaji.


Tel:- +255659594226,
         +255738651846,
         +255687466963.

www.wezamtima.comwezamtima@gmail.com

www.wezamtima.com


Nguvu ya fikra haina ukomo.



UPANA WA ELIMU.

                        UPANA WA ELIMU.            Kila swali katika dunia hii,           linaweza kujibiwa kwa majibu-            ...